Want create site? Find Free WordPress Themes and plugins.

Serengeti Boys kushiriki mashindano ya Aegean 2022.

Kikosi cha timu ya Taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 17 (U-17) Serengeti Boys kimeingia kambini tayari kujinoa na mashindano ya Aegean 2022 (Aeagen Cup Tournament), yanayotarajia kuanza kurindima Januari 15 huko nchini Uturuki.

Kikosi hiko kinachojumuisha wachezaji 30 kutoka mikoa mbalimbali kilipatikana baada ya mchujo wa Zaidi ya mara tatu kwa kucheza mechi na timu tofauti ili kupima uwezo wa wachezaji wenye viwango ambao  mwishoni walipata nafasi ya kuunda kikosi  hiko.

Akizungumza baada ya kumaliza mazoezi katika uwanja wa Karume  kocha mkuu wa Serengeti Boys Maalim Saleh alisema, mwaka huu wamepata wachezaji wengi wenye vipaji vya hali ya juu ukilinganisha na miaka mingine iliyopita, lakini pamoja na vipaji  vyao  bado kuna kazi kubwa ya kuwatengeneza na kuwaongezea baadhi ya mbinu ili wawe katika hali ya utayari wa mashindano hasa ukizingatia wengi ni wageni na hawana uzoefu  katika mashindano  ya kimataifa.

“ Mashindano ya Aegean sio mepesi kwa kuwa yanajumuisha timu nyingi bora kutoka mabara tofauti tofauti huku zikiwa zimesheheni upeo mkubwa  na wachezaji wake wamepata mafunzo  na wamekuzwa katika misingi ya soka  hivyo  ninaona kabisa ushindani  utakuwa  mkubwa jambo ambalo kwa upande wangu nitahakikisha mambo yote ya kiufundi na mbinu za kiushindani zinafundishwa na kueleweka kwa wachezaji ndani ya siku 10 ambazo watakaa kambini kabla ya kuianza safari  ya Uturuki” alisema Maalim.

Hii itakuwa ni mara ya tatu kwa Serengeti boys kushiriki mashindano hayo ambapo kwa mara ya mwisho walishiriki mwaka 2020  na kuibuka kuwa washindi wa tatu wakitoka sare na mwenyeji timu ya Uturuki, huku mwaka 2021 mashindano yakishindwa kufanyika kutokana na kuibuka kwa ugonjwa wa Uviko -19.

 

 

Did you find apk for android? You can find new Free Android Games and apps.